CHAMA
CHA WANAFUNZI WA KISWAHILI VYUO VIKUU VYA AFRIKA YA MASHARIKI (CHAWAKAMA)
OFISI
YA KATIBU MKUU CHAWAKAMA KANDA YA TANZANIA
S.L.P.
351901 DAR ES SALAAM (TANZANIA)
SIMU: 0777 445 569 (Mw/kiti)
0757 487 481 (Katibu)
Baruapepe: chawakama2014@yahoo.com
Baruapepe: chawakama2014@yahoo.com
Kwa
23/11/2014
Wanachama Wote wa
CHAWAKAMA
Kanda ya Tanzania.
YAH: TAARIFA YA MWALIKO WA KONGAMANO LA SABA (7) LA
KITAIFA LA
KISWAHILI NA MKUTANO MKUU WA CHAWAKAMA.
Tafadhali shufu mada tajwa hapo juu.
Ofisi ya Katibu Mkuu wa CHAWAKAMA Kanda ya Tanzania inayofuraha
kuwataarifu Wanachama wote wa CHAWAKAMA katika kanda ya Tanzania kuwa kongamano
la saba la Kitaifa la Kiswahili na Mkutano Mkuu wa CHAWAKAMA mwaka huu
linatarajiwa kufanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuanzia tarehe 23-25
Februari, 2015.
Hivyo basi, ninapenda kutumia fursa hii kuwaalika Wanachama wote
kuhudhuria katika Kongamano hilo ambalo ni muendelezo wa makongamano ya Kitaifa
ya CHAWAKAMA ya kila mwaka yanayofanyika kwa zamu katika Vyuo Wanachama.
Aidha napenda kutumia fursa hii kuwakumbusha viongozi wote wa matawi
kutoa taarifa kwa walezi na uongozi wa Chuo ili kupata ruhusa ya kushiriki
katika kongamano bila kuitilafiana na ratiba na taratibu za Chuo husika.
Nawatakia maandalizi mema ya kongamano.
Wenu katika kuienzi na kuikuza Lugha ya Kiswahili,
ATHANAS BARNABA B.
Katibu Mkuu wa CHAWAKAMA Kanda ya
Tanzania.
“KISWAHILI HAZINA YA AFRIKA
KWA MAENDELEO ENDELEVU”
No comments:
Post a Comment