Kurasa Muhimu

Friday, November 22, 2013

                         WANACHAMA, WADAU NA MASHABIKI WA BLOGI HII BILA SHAKA MNAENDELEA VYEMA NA MAJUKUMU YENU YA KILA SIKU IKIWA NI PAMOJA NA KUKIENZI KISWAHILI KAMA TUNU NA AMALI YA AFRIKA.
      
      Chuo kikuu cha Dar es Salaam kimepata bahati ya kutembelewa na nguli mtetezi wa lugha za Afrika, Prof. Ngugi wa Thiong'o Tar. 22 Novemba, 2013 ambapo alikuwa na kongamano na wanafunzi hapa chuoni katika ukumbi wa Nkurumah.
      Katika kongamano hilo Profesa Ngugi alisizitiza suala la lugha kuwa ni silaha ya kivita kwa jamii yoyote ile dhidi ya harakati za kuleta umoja na maendeleo, hivyo akawaasa wanazuoni na waafrika kuzitukuza na kuziendeleza lugha zetu ikiwa ni pamoja na kuikuza lugha ya Kiswahili ili iweze kuwa miongoni mwa lugha kubwa duniani kama ilivyo kwa lugha ya kiingereza, kifaransa kiarabu na nyingine kama hizo.
      Moja ya mifano yake ni pamoja na kuwaonya wanazuoni kutofanana na majemadari wa kivita ambao wametekwa na maadui huku raia wakitegemea ushindi kutoka kwao, kwani kutumia lugha za kigeni mfano kiingereza ambacho kinatumiwa na mabepari kama silaha ya kututawala, kama lugha ya kufundishia ili hali tuna lugha zetu za asili ya kiafrika, huku tukitegemea kuleta umoja na mshikamano ni kujidanganya na kamwe hatutoshinda kwani tunajenga tabaka la waliosoma yaani wanaojua kiingereza na wale wasio soma yaani wasiojua kiingereza. Je mlio wasomi mtafikishaje maarifa yenu kwa wale ambao hawakubahatika kuipata elimu hasa ya ngazi za juu?, kwa lugha ya kiingereza?, Na baada ya kuhitimu mnaenda kuhudumia jamii lugha ya aina gani?, ya wanaozungumza kiingereza?, Jibu kila mdau analo. Chondechonde ewe mzalendo chukua hatua madhubuti kuiokoa Afrika katika mateka hii ya lugha.
       Profesa Ngugi anatuhasa kuzitumia lugha zetu za kiafrika hasa lugha ya Kiswahili katika kutolea elimu na nyanja nyingine ili kufanikisha azma ya waasisi wetu kama Mwalimu J.K Nyerere, na Nkurumah ambao walikua na dhamira ya kuifanya Afrika iwe na lugha moja. kuhusu lugha za kigeni alisema zitumike kuongeza maarifa zaidi na maarifa hayo tuyatafsiri katika lugha yetu tukufu ili kila mzawa wa bara hili aweza kufaidika.
       kwa ufupi hayo ndiyo yaliyojiri katika kongamano hilo ambalo lilihudhuriwa na makamu mkuu wa chuo Profesa R. Mkandala,Timu ya wataalamu wa lugha toka TATAKI ikiongozwa na Prof. M.M. Mlokozi, Maprofesa kutoka vitivo na shule ndani ya chuo, madaktari,wahadhiri wakufunzi, na wadau mbalimbali wa lugha na fasihi pamoja na wanafunzi.  
                Kwa maoni, ushauri, pendekezo au swali kuhusu mawazo haya ya profesa Ngugi wa Thion'go usisite kuyatoa kwetu. ahsante. 
                                      Imeandaliwa na kuwasiliswa kwenu na,
                                                 mhariri mkuu
                                                         CHAWAKAMA CKD,
                                                                        Athanas Barnabas.   

3 comments:

  1. Kazi nzuri sana vijana, endeleeni kuchapa kazi

    ReplyDelete
  2. This comment has been removed by a blog administrator.

    ReplyDelete
    Replies
    1. ahsante kaka kwa pongezi zako na maneno ya kutotia hamasa, kwa pamoja tutaifikisha mbali ukurusa wetu.

      Delete