Kurasa Muhimu

Saturday, June 14, 2014


Wahitimu wa CHAWAKAMA-CKDSM 2014 wakiwa katika picha pamoja na Mkurugenzi wa TATAKI Dr. Mosha ambaye pia ni Mlezi wa chama, baada ya kutunukiwa vyeti vyao vya uanachama.



UONGOZI MPYA WA CHAWAKAMA.

Baadhi ya viongozi wapya wa CHAWAKAMA- CKDSM 2014/2015  wakiwa katika picha ya pamoja. Kutoka kushoto ni Malcelino Dee(Mahazini Msaidizi), Mgata Visa(Katibu Mkuu), Athanas Barnaba(Mwenyekiti), Sarah Uvumbe(Makamu Mwenyekiti) na Joel Nkoma(Mhariri Mkuu)

Thursday, May 15, 2014


MADA ZA KONGAMANO

KAULI MBIU YA KONGAMANO NI
“KISWAHILI MALIGHAFI YA UMOJA WA AFRIKA MASHARIKI”

Kauli mbiu hii inalenga kuhimiza umoja na utangamano wa nchi za Afrika Mashariki.Lugha ya Kiswahili ina mchango mkubwa sana katika kuleta utangamano,umoja na mshikamano mwema baina ya nchi za Afrika Mashariki.Kando na mchango wa  Biashara,Michezo na Elimu.Swali ni je,Lugha ya Kiswahili ina mchango wowote katika mchakato wa kuimarisha na kukuza vipengele hivi vitatu; umoja,utangamano na mshikamano.

1.      Kiswahili ni lugha mwafaka ya umoja wa Afrika mashariki.
2.      Nafasi ya lugha ya Kiswahili katika tamaduni za nchi za Afrika Mashariki.
3.      Kiingereza au Kiswahili? Katika mwamko mpya wa Afrika Mashariki huru.
4.      Kiswahili na michakato ya kisiasa katika nchi za Afrika mashariki.
5.      Nafasi ya Kiswahili katika sanaa ya kisasa (Karne ya ishirini na moja).
6.      Mchango wa lugha ya Kiswahili katika upanuaji na uendelezaji wa elimu ya juu Afrika Mashariki.
7.      Kiswahili na uimarishaji wa usalama katika ubia Afrika mashariki.
8.      Changamoto za kisiasa,kiuchumi na kiusalama katika lugha ya Kiswahili,
9.      Ubunifu na talanta katika uzalishaji wa kazi mufti  ya fasihi ya Kiswahili
Lugha  ya Kongamano: Lugha rasmi ya Kongamano ni Kiswahili. Makala yaliyoandikwa kwa Kiingereza yatakubaliwa tu iwapo hapana budi.wajumbe wanashauriwa kuanda makala yao katika lugha ya kiswahili
Ikisiri: Ikisiri za kati ya maneno 200-300 zitumwe  kabla ya tarehe 30 Mei 2014 kwa Mratibu wa Kamati ya Maandalizi kupitia barua meme kwenye anwani ifuatayo: Billysakwa@gmail.com,AU Mhariri Mkuu godwinalex664@yahoo.com (+255718252853) au kwa katibu mkuu wa chawakama Afrika mashariki Ahamadi Jumbe. Chawakama.am@gmail.com .
Makala: Makala kamili ya ikisiri zitakazokubaliwa yatumwe kwa Mratibu kwa baruameme kufikia tarehe 30 Juni  2014 kupitia anwani ifuatayo: Billysakwa@gmail.com

Ili kupata nafasi ya kuwasilisha makala uliyoandaa ni lazima.mjumbe atume ikisiri na hatimaye makala kamili ya mada aliyoandaa.Makala haya yatachapishwa katika chapisho la makala la kongamano kabla ya tarehe 15 Julai 2014 .utaratibu na mpangilio wa uwasilishaji utatolewa tarehe 30 Julai 2014.

TANGAZO  TANGAZO  TANGAZO.

UONGOZI  WA  CHAWAKAMA  TAWI  LA CHUO  KIKUU CHA DAR ES SALAAM  UNAPENDA  KUWATANGAZIA  WANACHAMA NA  WADAU  WOTE WA LUGHA ADHIMU  YA  KISWAHILI  KWAMBA  KUTAKUWA  NA KONGAMANO LA KUMI  LA KIMATAIFA.
KONGAMANO HILO LITAFANYIKA NCHINI KENYA KATIKA CHUO KIKUU  CHA LAIKIPIA  KUANZIA  TAREHE  21/ 08/2014  MPAKA  TAREHE  24/08/2014.  WASHIRIKI WA KONGAMANO WATATOKA KATIKA KANDA ZOTE AMBAZO NI WANACHAMA WA CHAMA HIKI AMBAZO NI TANZANIA, KENYA, UGANDA,RWANDA, BURUNDI NA KONGO.
MADA MBALIMBALI  ZINAZOHUSU  LUGHA YA KISWAHILI  ZITAWASILISHWA NA KUJADILIWA KATIKA KONGAMANO HILO, AMBAZO ZINAGUSA SANA SUALA LA UMOJA NA USHIKAMANO MIONGONI MWA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI.

KAULI MBIU.
KAULIMBIU  ITAKAYOLIONGOZA KONGAMANO HILO NI:

KISWAHILI MALIGHAFI  YA UMOJA WA AFRIKA MASHARIKI.
GHARAMA.

  1. KILA MSHIRIKI ANAPASWA KUTOA FEDHA TASLIMU KIASI CHA SHILINGI ELFU HAMSINI NA TANO (55,000/=) ZA KITANZANIA KWA AJILI YA CHAKULA, MALAZI, FULANA NA CHETI CHA USHIRIKI. FEDHA HIYO ITAKUSANYWA KABLA ILI IWASILISHWE KWA VIONGOZI HUSIKA KWA AJILI YA MAANDALIZI YA KONGAMANO.
  2. KILA MSHIRIKI ATAPASWA KUJITEGEMEA KWA GHARAMA ZA USAFIRI WA KWENDA NA KURUDI, NA KUAANDAA HATI YA KUSAFIRIA.                                                                                                                                                                                                     KWA SASA VIONGOZI WAPO KWENYE MCHAKATO WA KUWAANDIKISHA WOTE WATAKAOPENDA KUSHIRIKI, ILI ZOEZI LA KUANDAA HATI ZA KUSAFIRIA LIANZE MARA.                                                                                                                                           HIVYO, NI VYEMA UKAJIANDIKISHA SASA KWA VIONGOZI AMBAO WANAHAMASISHA KATIKA MIHADHARA MBALIMBALI. KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NA VINGOZI KWA NAMBA ZIFUATAZO.
MWENYEKITI         0757487481
KATIBU                    0757794239
MHAZINI                  0655832600
MHARIRI                  0769978920

Friday, April 4, 2014


Picha Na. 01 Wawasilishaji wa mada kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam Pacho na Geniva wakiwasilisha mada ya Shaban Robert ambayo pia ilirekodiwa na mwandishi wa habari wa TBC1 ndugu Victor Eliah kwa ajili ya kurushwa hewani kama kipindi katika runinga ya taifa ya TBC1. 


TANBIHI: PICHA HIZI NI MIONGONI MWA MATUKIO YALIYOJIRI KATIKA KONGAMANO LA CHAWAKAMA KANDA YA TANZANIA LILILOFANYIKA KATIKA CHUO CHA ECKERNFORDE-TANGA FEBRUARI 2014.





Picha Na.02 washiriki wa kongamano wakiwa katika maandamano kuelekea ukumbini katika siku ya ufunguzi wa kongamano.

 Picha Na. 03: miongoni mwa wanachama wakiwa eneo la kaburi la marehemu Shaban Robert.